Ni hali ya kuharibika kwa nevu ya kuona inayounganisha jicho na ubongo inayotokana na presha kubwa ndani ya jicho.
Hakuna dalili za dhahiri za mwanzo za glaukoma. Baadaye mgonjwa huanza kupoteza uwezo wa kuona taratibu.
Uwezo wa kuona uliopotea kutokana na glaukoma hauwezi kurudishwa ila dawa, tiba ya mionzi na upasuaji inaweza saidia kuzuia jicho kupoteza zaidi uwezo wake wa kuona.